TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749

            
Mahakama nchini Uganda imemhukumu kwenda jela miaka minne mfanyakazi wa ndani (House girl) Jolly Tumuhiirwe aliyepatikana na hatia ya kumtesa na kumpiga mtoto mwenye miezi 18. Katika video iliyosambaa mitandaoni hivi karibuni, House girl huyu alionekana akimpiga bila huruma mtoto Aneela. Mfanyakazi huyo alijitetea na kusema hakujua nini kilitokea hadi kufikia kufanya unyama huo

0 comments :

 
Top