TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749



By Kosseyi  Deogratius,sjmc

Real Madrid ni moja kati ya klabu kubwa sana duniani.Ni klabu yenye utajiri,heshima na historia kubwa.Klabu ambayo imetwaa ubingwa wa  ulaya mara kumi na mataji lukuki ya la liga.Kutokana na historia iliyonayo Real Madrid,imekuwa ni kiu ya kila mwanasoka kuchezea kikosi hicho cha Santiago Bernabeu.

Sera kubwa ya klabu hii ni kusajili wachezaji wenye majina makubwa.Wachezaji wa kariba ya Zinedin Zidane,Luis Figo,David Becham,Ronaldo de Lima ndio wanaohitajika Madrid kwa dau lolote lile.

Rais wa real Madrid Ferentino Perez ni mtu mwenye nyodo sana.Shauku yake ni kuona wachezaji aliowanunua kwa gharama kubwa wakicheza pamoja kwenye kikosi cha kwanza.Mara nyingi makocha wanaokwenda kinyume na mtazamo huu wa Perez,vibarua vyao vinakuwepo shakani.

Hii ndiyo sababu inayomlazimu mtaalamu Carlo Ancelloti kuwaanzisha kwa pamoja Christiano Ronaldo,Karim Benzema,Gareth Bale na James Rodriguez huku akifahamu kuwa timu inakosa utimamu katika kukaba pindi inapopoteza mpira.Katika mfumo wa 4:3:3 nafasi ya kiungo inaongozwa na Toni Kroos,Isco na James Roriguez.Kimsingi Rodriguez ni mshambuliaji.Toni Kroos na Isco ni viungo washambuliaji kwa asili.Ukiwachukua kwa pamoja Ronaldo,Bale,Benzema,Rodriguez,Isco na Kroos unakuwa na timu ambayo ina wachezaji  sita ambao akili yao ipo katika kushambulia.Hapa unatengeneza tatizo katika ukabaji kwani kunakosekana uwiano wa kukaba na kushambulia.Timu inakuwa imara katika kushambulia lakini inakuwa dhaifu katika kuzuia.

Kwanini Ancelloti anapanga kikosi kwa namna hii? Zipo sababu kuu mbili,ambazo kwanza ni kumfurahisha Ferentino Perez anaetaka kuona mastaa wake wakicheza pamoja uwanjani,mastaa ambao amewanunua kwa pesa ndefu.Lakini pili Ancelloti anatupangia timu kwa mantiki hii kwasababu anajua La Liga ina mechi ngumu mbili ambazo ni dihi ya Barcelona na Atletico Madrid.Katika ligi ambayo timu inaweza kushinda mechi 18 mfululizo na kubeba ubingwa ukiwa na point 100,ni rahisi mno kupanga kikosi chenye wachezaji sita ambao kukaba ni jukumu lao la dharura.

Ukweli ni kwamba Madrid ni hodari mno kwenye kushambulia.Katika nafasi tano wanazoweza kupata,uwezekanao wa kufunga magoli matatu ni mkubwa sana.Hii ndiyo silaha kubwa waliyonayo katika kuamua matokeo ya mechi.

Real Madrid wana shimo kubwa kwenye safu ya kiungo hasa kipindi hiki ambacho fundi Luka Modric akiuguza majeraha.Lakini shimo hili linafukiwa na safu kali ya ushambuliaji.Kwa haraka huwezi kuliona shimo hili.Tunahitaji timu yenye safu kali ya viungo wenye vurugu,utimamu wa mwili na uwezo wa kukaba watuonyeshe shimo hili.Watuonyeshe udhaifu huu unaofanana na Argentina ya Maradona ya mwaka 2010 ambae alikuwa akitupangia kwa pamoja Messi,Aguero,Tevez,Higuain na Di maria na hatimae wakaadhiriwa na Ujerumani kwa mabao 4:1 katika hatua ya robo fainali ya kombe la dunia.

Je, Ancelloti ataipanga Madrid kwa mtindo huu katika hatua ya mtoano  ya Eufa Champions League? Ni swala la muda,tusubiri tutaona.

0 comments :

 
Top