LEO mgombe urais kupitia UKAWA
kwa tiketi ya CHADEMA, Edward Lowassa amesema kuwa Mtatiro anafaa kuwa
mwakilishi wa wananchi wa jimbo la Segerea na kuwa msimamizi wa vipaumbele 11
vya serikali yake endapo atashinda uchaguzi huu ambao anaimani atashinda.
Aliyasema hayo alipokuwa
akihutubia katika mkutano wa jimbo la Segerea, ambako alivitaja vipaumbele
vyake kuwa ni, kufuta michango na ada kuanzia chekechea hadi chuo kikuu,
kukusanya kodi bora na rafiki kwa wajasilia mali wadogo wadogo, kuunda tume ya
kutatua migogoro, kupunguza kodi za mishahara ya wafanya kazi, kuboresha
maslahi ya polisi na usalama, kupunguza foleni ya magari kwa jiji la Dar es
salaam.
Aliongeza kuwa atatatua kero za boda
bod, mama ntilie na wafanya biashara wadogowadogo, kukuza michezo na sanaa,
kuunda tume ya kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji, kuanzisha kituo cha
kushughulikia matatizo ya wannchi kwa kila mkoa, kutengeneza mkakati wa kutatua
kero za maji kwa nchi nzima. Pia aliwataka wannchi kukubari kuwa mda wa
mabadiriko umefika.
“nimezunguka katika mikoa 23,
kila mkoa unataja mabadiliko tu, si mjini na si vijijini. Kila mtu yuko tayari
kwa mabadiliko. Nataka mabadiliko hasa kwenye elimu ili vijana wetu wawe na
ushindani katika soko la ajira duniani. Ninacho wasisitiza ni kupiga kura kwa wingi
na kuhakikisha mnalinda kura zenu” amesema Lowassa.
Kwa upande wake Mtatiro alisema
kuwa irani ya UKAWA ndio suluhu ya kero zote za wananchi, hivyo wannchi hawana
budi kuipa kuara yandio UKAWA kuanzia udiwani ubunge hadi urais.
Lowassa amefanya mikutano mine ndani
ya Dar es salaam, ikiwa ni Jimbo la Segerea, jimbo la Temeke, jimbo la Ubungo
na jimbo la Kawe ambako watu wengi walijitokeza kumsikiliza sera zake na akiwanadi
wagombea ubunge na udiwani katika majimbo hayo.
| Mtatiro akiwa na aliyetangaza nia ya ubunge kupitia CHADEMA lakini baada ya makubaliano ya UKAWA amekubali kumuachia Mtatiro kupitia CUF jimbo la Segerea |
| Makongoro Mahanga, akimuombea kura za ushindi Mtatiro kwa wananchi, ili awe mrithi wake |
0 comments :
Post a Comment