TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749

Katibu Mkuu Kiongozi Ombeni Sefue ametangaza baraza jipya la mawaziri lenye sura nyingi mpya na wengine wameachwa.

A: Saada Mkuya awa waziri wa fedha manaibu ni Mwigulu Nchemba na Adam Malima....

B: Wizara ya Sheria na Katiba amepewa Dr Asha-Rose Migiro na naibu wake ni yule yule Angela Kairuki

C: Wizara ya Elimu waziri ni Shukuru Kawambwa na naibu ni Jenister Mhagama. Philip Mulugo ameondolewa kabisa serikalini

D: Wizara ya Mifugo na maendeleo ya uvuvi waziri ni Dr Titus Kamani, Naibu wake ni Kaika Telele. Ole Nangolo ameondolewa serikalini.

E: Wizara ya Maendeleo ya jamii jinsia na watoto, Waziri ni Sophia Simba, naibu wake ni Pindi Chana, Umy Mwalimu amehamishiwa Muungano.

F: Wizara ya Ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi waziri ni Anna Tibaijuka, Naibu ni George Simbachawene

G: Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika waziri ni yuleyule Christopher Chiza na naibu ni Godfrey Zambi. Adam Malima amehamishiwa wizara ya Fedha

H: Wizara ya Nishati na Madini, waziri ni yuleyule Prof Muhongo, manaibu ni Steven Maselle na Charles Kitwanga. Simbachawene yuko Ardhi

I: Wizara ya Maliasili na Utalii waziri ni Lazaro Nyalandu na naibu wake ni Mahamoud Mgimwa mbunge wa Mufindi Kaskazini

J: Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Waziri ni yuleyule Dr. Fenella Mukangara, naibu ni Juma Nkamia mbunge wa Kondoa Kusini.

K: Wizara ya Mambo ya ndani waziri ni Mathias Chikawe aliyekuwa sheria na katiba, na naibu wake ni yuleyule Pereira Sillima.

L: Wizara ya Afya aliyekuwa naibu Dr. Seif Rashid amekuwa waziri na naibu wake ni Mbunge wa Serengeti Kebwe Stephen Kebwe.

M: Wizara ya Ulinzi na JKT Waziri ni Dr Hussein Mwinyi aliyekuwa Waziri wa Afya

N: Wizara za Uchukuzi, Ujenzi, Ofisi ya Rais, Ofisi ya waziri Mkuu Mambo ya nje, Afrika Mashariki, Mawasiliano, Kazi. Hakuna mabadiliko

Wizara ambazo hazina mabadiliko ni: Wizara za Uchukuzi, Ujenzi, Ofisi ya Rais, Ofisi ya waziri Mkuu ,Mambo ya nje, Afrika Mashariki, Mawasiliano na wizara ya Kazi.

Sura mpya katika baraza lililotangazwa ni:- Mwigulu Nchemba, Stephen Kebwe, Pindi Chana, Zambi, Juma Nkamia, Kaika Telele, Jenister Mhagama, Mahmoud Mgimwa na Dr. Migiro
See More

0 comments :

 
Top