The service to Widows Ophans ans the
Little one Organisation (SWOLO) ni asasi isiyokuwa ya kiserikali iliyosajiliwa
na inatambulika kisheria iliyoko wilayani Kyela Mkoa wa Mbeya,
inayojishughulisha na masuala ya kijamii hasa kusaidia wanawake wajane wazee
kuanzia miaka 60 na kuendelea, watoto yatima ammbao walezi waohawana uwezo,
watoto wadogo (wtukutu).
Asisi hii inaongozwa na Murugenzi
Abel Ambakisye, ambaye amekuwa akifanya kazi ya kuhamasisha na kutoa ushauri
kuhusu haki za wazee. Lakini pia asasi
inamlezi ambaye ni mwanasheria Mhe. Jaji mstaafu Raymund Mwaikasu ambaye
amekuwa mshauri mkubwa saana kwa asasi hii.
Asasi hii ilianza kufanya kazi mnamo
tarehe 15/06/1995 kwa kulitangazia taifa tatizo la watoto yatima kwa uzito mno
kupitia redio tanzania dar es salaam kwa wakati huo, ITV, na katika vyombo vya
habari vingine kama vile magazeti. Hii ilfanya jamii kuamuka na kuunda ASASI
zilizo jitokeza kusaidia watoto yatima na baadhi ndio hizi zinazoendeshwa mpaka
sasa.
ASASI hii ilishindwa kufikia malengo
yake ya kuwaweka pamoja watoto yatima na kujenga zahanati za kuwahudumia
walengwa kutokana na kukosa misaada ya kutosha kutoka kwa jamii na kujikuta
ikiwa katika upande wa utetezi na,
ushawishi na ushauri kwa walengwa.
SWOLO ilikuwa chachu kwa jamiii kujua
zaidi umhimu wa ASASI na kufungua ASASI nyingi nchini ambazo zilikusudia
kusaidia watoto yatima na watoto wa mitaani.
MAFANIKIO YA ASASI
Mnamo mwaka 2000 SWOLO iliteuliwa
kimkoa kuziwakilisha asasi zisizo za
kiserikali kushiriki katika warsha iliyokuwa imeundwa nashirika la kimataifa la Help Age
linalotetea haki za wazee kwa ujumla.
Akielezea hatua hiyo Mkurugenzi wa
SWOLO, Ambakisye alisema kuwa waliteuliwa kwa sababu ni ilikuwa ni asasi
iliyokuwa inautendaji m zuri kwa jamii na ushirikiano mzuri na shirikak hilo la
Help Age na mpaka sasa wanaendelea na ushrikiano huo.
Pia mwaka 2003 asasi hii ilishiriki
warsha ambayo iliitishwa na shirika la Help Age iliyo shirikisha TUME YA HAKI
ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA nchini ikihusu HAKI ZA WAZEE.
Asasi hii ni ya kwanza kuanzisha
mafunzo ya awali ya kidato cha kwanza kwa wilaya wa Kyela huku ikianzisha pia
darasa la Elimu ya watu wazima likiwahusisha watumishi wengi walioishia darasa
la saba..
Mafanikio makubwa hasa ambayo ni ya
kujivunia kwa asasi hii na jamii kwa ujumla ni kuunda mabaraza ya wazee katika
kila kijiji na kila kata huku kukiwa na viongozi wanaoyaongoza mabaraza hayo
kuanzia ngazi ya kijiji hadi ngazi ya kata.
Pia imefanikiwa kutetea na kutoa
elimu kuhusu mambo makubwa mawili yaliyomo katika sera ya serikali
·
Matibabu
bila malipo kwa wazee wote wenye umri kuanzia 60 na kuendelea tofauti na hapo
nyuma ambaposerikali ilidai kuwasamehe wazee wasiojiweza tu.
·
Penseni
ya kinga (protection pension) kwa wazee wote ambao ni Watanzania kuanzia miaka
60 na kuendelea bila ya kujali sekta yake ya utumishi kwa umma uma wetu, aidha
Mkulima , Mvuvi, Mfugaji, Mtumishi wa Kanisa, Mfanyabiashara N.K
KWA MCHANGO
WAKE WOTE HUO ASASI HII INATAKIWA KUKUMBUKWA NA KUPEWA USHIRIKIANO ZAIDI ILI
IZIDI KUFANYA KAZI ZAIDI YA KUTETEA WAZEE NA WAJANE.
Kwa
mawasiliano na SWOLO
Telephone +255
2540320
Mobile +255 787413200
+255 759371317
Email swolo1992@yahoo.co.uk
0 comments :
Post a Comment