TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749

Sir Robert "Bobby" Charlton alizaliwa 11 Oktoba 1937 ni mchezaji wa zamani  wa mpira wa miguu wa Uingereza, Anajulikana kama mmojawapo wa viungo  wa kati  wenye uwezo wa hali ya juu wa muda wote, nembo muhimu  katika timu  ya taifa ya Uingereza ambapo alishinda Kombe la Dunia  na  Ballon d'O r mwaka 1966. Yeye alicheza karibu muda wote katika klabu yake soka ya Manchester United, ambapo alikuwa mashuhuri kwa uwezo wake wa  kushambulia na kupiga mashuti yaliypachikwa jina "long range shot" yaliyopigwa toka umbali mrefu. Alionywa kwa kadi mara mbili tu katika maisha yake ya soka; mara moja dhidi ya Argentina mwaka 1966 katika  Kombe la Dunia, na  katika mechi ya ligi kuu  dhidi ya Chelsea.

Alizaliwa huko Ashington, Northumberland, Charlton alicheza mechi yake ya kwanza kwa Manchester United katika kikosi cha kwanza mwaka 1956, na zaidi ya misimu miwili alipata nafasi ya uhakika katika timu,  ni mmoja wa wachezaji walionusurika katika ajali ya anga mjini  Munich mwaka 1958 baada ya kuokolewa na Harry Gregg, baada ya kuisaidia Mashetani Wekundu  kushinda kombe la Football League  mwaka 1965, alishinda Kombe la Dunia  na medali katika timu ya taifa ya Uingereza mwaka 1966 na kombe la  Football League akiwa na  Mashetani Wekundu  mwaka uliofuata. Mwaka 1968, akiwa nahodha wa Manchester United  alishinda Kombe la Ulaya, akifunga mabao mawili katika mechi ya fainali . Amefunga mabao zaidi kwa United  (249) kuliko mchezaji mwingine yeyote na kutokea  kuwa  mfungaji bora England  wa muda wote, kwa timu ya Taifa mabao(49).
Hivyo  kuanzia Mei 1968 hadi Septemba 2015, kwa Rooney kuvunja  rekodi hiyo ndani ya  Uingereza. Bobby Charlton alikuwa na  rekodi ya kucheza  mechi nyingi kwa Manchester United (758),  kabla ya kuzidiwa  na Ryan Giggs.

Aliichezea Uingereza mara  nne katika  Kombe la Dunia (1958, 1962, 1966, na 1970), na kuisaidia Uingereza kushinda shindano hilo mwaka 1966.
 Wakati wa kustaafu wake kutoka timu ya England mwaka 1970, alikuwa ameichezea timu ya Taifa mechi nyingi kuliko mchezaji yeyote , mara 106 katika ngazi ya juu. Rekodi hii tangu wakati huo ilikuwa kwa upande  wa Bobby Moore na Peter Shilton.

Aliondoka Manchester United na  kuwa meneja wa Preston North End katika  msimu  wa 1973-1974.  Ambapo alikuwa  mchezaji-meneja msimu uliofuata, na baadaye kuwa mkurugenzi wa Wigan Athletic, akawa mwanachama wa bodi ya wakurugenzi  Manchester United tangu  mwaka 1984 mpaka sasa msimu wa 2015/16.
Huyu ndiye Sir Robert  "Bobby" Charlton aliyeshikilia rekodi ya ufungaji wa mabao Uingereza kwa miaka 47!

0 comments :

 
Top