TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749


Didier Drogba, afunguka nakudai anatamani kuwepo tena klabuni Chelsea kwa mara nyingine akiwa kama kocha.
 Mshambuliaji huyo wa    Ivory coast  anayekipiga katika klabu ya Montreal Impact   kwa soka la kulipwa huko Canada, na ambaye  aliifungia “the blues” mabao 164 katika maisha yake ndani ya Stamford Bridge athibitisha hamu yake ya kurudi Chelsea kama mkufunzi katika utambulisho wa kitabu chake kiitwacho “Commitment”.
 Drogba ambaye  bado ni shujaa kwa “the blues” kwani aliifungia bao lililoipa ushindi na taji la mabingwa wa bara Ulaya mwaka wa 2012, amedai  kuwa angependa kuihudumia klabu hiyo hata baada ya kukamilika kwa kipindi chake cha uchezaji.
Muivory coast huyo alithibitisha kuwa  tayari nimekubaliana na Wakurugenzi wa klabu hiyo kuwa ana uwezekano wa  kurejea kuwa mkufunzi kwa sababu klabu hiyo inamfaa sana.
Tembo huyo pia alizungumzia uwepo wa uongozi mzuri kati ya wachezaji kwa kumtolea jicho la undani zaidi nahodha John Terry kuwa yupo pekee yake mkongwe  kwa kudai enzi zao hawakupoteza michezo kirahisi kama sasa ambapo Chelsea imepoteza michezo 7 kati ya 13 huku wakiwa vnyuma ya Arsenal kwa pointi 12 kwa kuwa kipindi chao walikwepo wachezaji mahiri wenye nguvu ya ushawishi kama yeye, Michael Ballack, Andriy Shevnchenko, John Terry, Makelele, Michael Essien na wengineo.
Kuhusu suala la uongozi alihoji ''Kwani haiwezekani kuwa meneja? siwezi kuwa mkurugenzi wa kiufundi, mkufunzi wa chuo cha mafunzo ya wachezaji ama hata mshauri wa washambuliaji?  alisema mshambuliaji  huyo mwenye umri wa miaka 37.




Kuhusiana na nafasi ya waliopo Chelsea, tembo huyo wa Afrika Magharibi amedai  bado kocha wake Jose Mourinho ni “special” kwake kwa uhusiano na na uwezo alio nao lakini hakusita kumtaja kocha bora aliyewahi kukutana na  kupambana na vijana  na wake  katika  maisha ya soka kuwa Sir Alex Ferguson enzi zake Old Trafford.

Drogba alikwenda mbali nakudai kikosi cha Arsenal kina uwezekano wa kuchukua ubingwa wa England msimu huu kwa kuamini rafiki yake Petr Cech waliyecheza nae Stamford Bridge  kwa ukongwe atakuwa nafasi nzuri kuchukua vikombe ndani ya kikosi cha “the Gunners”.
Kwa upande wa timu bora aliyopambana nayo ni Barcelona huku akiwahusudu Ronaldinho, kiungo wa zamani wa Barcelona na timu ya Taifa ya Brazil, Lionel Messi na Zinedine Zidane kuwa moja kati ya wachezaji wa kiwango cha juu aliowatamani kuwa kikosi kimoja na wao.

0 comments :

 
Top