TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749

Mgombea urais kupitia chama chaNational Resistance Movement (NRM), Yoweri Museveni ameahidi ruzuku kwa wakazi wa wilaya ya Wakiso itakayotumika katika kuleta maendeleo katika eneo hilo.
Museveni pia amewahakikishia Waganda kuwa uchaguzi utafanyika kwa amani na kwa wale waliona mpango wa kuvuruga amani atawasambaratisha ndani ya muda mfupi.
Pia Museveni amewaambia wafuasi wake kwamba serikali yake itapambana na tatizo la rushwa na kuwashughulikia  mara moja wale wote wafujaji wa rasilimali za taifa katika kipindi chake cha uongozi.
Kuhusiana na  masuala ya ukosefu wa ajira kwa vijana, amelaumu ukosefu wa ujuzi pia ameahidi kutoa shillingi billioni 500 kwa kusaidia vijana wasiokuwa na ajira na pia kujenga taasisi ya kiufundi katika kila jimbo nchini Uganda.

Source ( Gazeti la Daily Monitor) toka nchini Uganda.

0 comments :

 
Top