TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749

Rais wa Marekani Barack Obama amesaini sheria yenye lengo la kupanua umeme kwa mamilioni ya kaya Kusini mwa jangwa la Sahara na yenye kuokoa maisha na kuongeza kasi ya ukuaji barani Afrika.
Sheria hiyo ilipitishwa kwa kauli moja na Baraza la Wawakilishi, Seneti na kwa kushirikiana na sekta binafsi ambapo watahakikisha upatikanaji wa umeme kwa watu milioni 50 katika sehemu ya Afrika.
Serikali ya Marekani imeahidi kutoa  fedha kwa ajili ya mradi ambao utatumia mfumo wa dhamana ya mkopo kwa kuongezaa megawati 20,000 za umeme wa gridi ya bara hilo la Afrika  ifikapo mwaka 2020.
Hatua hiyo inatarajiwa kuwa itachochea ukuaji wa uchumi na kuboresha upatikanaji wa elimu na afya ya umma.

"Familia nyingi zitapumzika kutumia mkaa au vyanzo vingine vyenye sumu". anadai  Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje ndugu Royce.

Hatua hii ya Rais Barack Obama ya kusaini sheria ya mradi wa umeme uitwao ‘Power Africa’ ni kati ya ahadi alizotoa pindi alipotembelea nchini Kenya mnamo mwezi wa saba mwaka 2015.


Source (gazeti la Daily Nation) toka nchini Kenya

0 comments :

 
Top