TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749




Riyad Mahrez ni winga wa kimataifa wa Algeria alizaliwa miaka 24 iliyopita, mjini Sarcelles nchini Ufaransa mnamo tfebruari 21, 1991.
Alianza maisha yake ya soka katika kituo cha AAS Sarcelles akiwa na miaka 12 na ilipotimu mwaka 2009 Mahrez alifanikiwa kujiunga na timu ya Quiemper kama winga na kuifungia magoli mawili kwa msimu mmoja yaani 2009/2010.
Mzaliwa huyo wa Ufaransa mwenye asili ya Algeria aliamua kuichezea timu ya Taifa ya Algeria kwa kuvunja miiko ya wachezaji wengi kuchezea nchi walizozaliwa pasipo kuangalia asili ambapo aliiwakilisha Algeria kwenye mashindano ya kombe la dunia nchini Brazili pamoja na mashindano ya mataifa ya Afrika  mwaka 2014. Kutokana na kiwango alichokionyesha alipata ofa ya kuichezea PSG na Marselle za   Ufaransa na kuishia kukubali ofa ya kuwepo katika klabu ya Le Havre na kusaini mkataba wa miaka mitatu, kuicheza mechi za mashindano 60 na kufunga magoli 6.


Nyota ilipozidi kung’aa, mwaka 2014  akaangukia mikononi mwa klabu ya Leicester City ya nchini Uingereza iliyokuwa ikishiriki daraja la kwanza maarufu kama Championship League (kwa sasa inashiriki ligi kuu), mechi yake ya kwanza ilikuwa tarehe 25, mwezi wa kwanza 2014 ambapo alichukua nafasi dakika ya 79 akibadilishana na Lloyd Dyer  dhidi ya Middlesbrough ambapo walishinda mbili kwa bila.
Ujio wake kwa mara ya kwanza kwenye ligi kuu ya Uingereza umekuwa wa Baraka pia kwa klabu yake ya Leicester iliyopanda ligi kuu kwani ipo vyema  tangu alipoanza kucheza ligi kuu tangu agosti 18, 2014 na goli lake la kwanza alifunga dhidi ya Burnley Oktoba 10, 2014 walipotoka sare ya goli mbili kwa mbili
Msimu wa 2014/2015  umekuwa poa kwake kwa kufunga magoli manne na “ assists” 30, na kusaini mkataba wa miaka minne klabuni hapo kwa kiwango bora kilichomkuna Mkurugenzi wa klabu hiyo Nigel Pearson.
Kwa uwezo wake sio mbaya kwa sasa kuwa na goli 14 katika ligi kuu msimu huu wa  2015/2016 na mpaka sasa klabu inaongoza ligi kwa pointi 38.


0 comments :

 
Top