MASTAA mbalimbali nchini wakiwemo wanamziki, wanatarajiwa
kushiriki kwenye tukio maalum la kukumbukumbu ya mwaka mmoja tokea kifo cha
marehemu Albert Mangwea (Ngwair)
litakalofanyika ndani ya ukumbi wa Nyumbani Park (Samakisamaki Sport), Kihonda
Morogoro mjini, kesho Jumatano Mei 28 mwaka huu.
Ratibu mtendaji wa tamasha hilo, Kareem Omary “KO”, amesema
maandalizi ya tukio hilo litakalokuwa la kila mwaka, limepewa jina la ‘LOVE
CONCERT-KUMBUKUMBU YA KIFO CHA ALBERT MANGWEA’
Kareem amewaomba wadau kujitokeza kwa wingi kuunga mkono
kwenye tukio hilo kwani litakuwa la kipekee na la aina yake, ambalo pia litatoa
fursa nyingi kwa wakazi hao na mikoa ya jirani na watu kutoka nje ya Tanzania
ambao wataudhuria.
”Nawaomba wadau kujitokeza kuonesha upendo wa pamoja ,
kumbukumbu kwa mpendwa wetu kama ilivyo utamaduni wetu” alisema Kareem, na
kuongeza kuwa, siku hiyo Watu mbalimbali watapata kupiga picha na mastaa
mbalimbali pamoja na mama mzazi wa Mangwea.
Kareem aliwataja wasanii watakaotoa burudani kuwa ni pamoja
na, kundi la Wanachemba, wasanii toka morogoro: Afande Sele, Mc Koba, Chris wa
Marya, Belle 9, Samir, Zombie, President Mirrow, Jordan wa Dejavu, na wengine
wingi.
Kareem alisema Kabla ya show kuanza kutakuwa na kutakuwa na
ibada maalumu ikiwemo ya kanisani nay a Nyumbani.
AIdha Kareem aliongeza kuwa katika tukio hilo ambalo
lina[ptarajiwa kuaanza majira ya saa 10 hadi saa 12 jioni, wametoa fursa kwa
watoto kutoa burudani, ikiwemo ya kuimba na nyinginezo na baadae kuanzia saa 2
hadi majogoo wasanii hao mbalimbali watatawala jukwaa na kudondosha burudani ya
nguvu pande za ukumbini.
0 comments :
Post a Comment