Mkali wa muziki wa kughani (mashairi) nchini Mrisho Mpoto,
amezungumzia tuhuma zinazoelekezwa kwake kuhusu kutumika kisiasa na
kulaghai jamii, amedai si za kweli na zina lengo la kumchafua.
Akifunguka kupitia kipindi cha “the jump off” cha Times fm, Mpoto
amedai shughuli nyingi anazozifanya kiserikali ni za kuhamasisha jamii
katika maswala ya Elimu, Afya na maendeleo zaidi.
“Unajua mi nashindwa kuelewa, kwa mfano nikienda Kigoma kuhamasisha
wananchi juu ya maswala ya kutumia Chandarua kuepuka malaria kuna tatizo
gani? nikihamasisha watu wajiunge na bima za Elimu kunatatizo gani?,
mimi situmiki eti kuwafunga midomo wananchi hapana, wala situmiki
kisiasa nafanya vitu kwa maendeleo ya jamii ni watu tu wanaona kama
natumika na chama Fulani eti” alisema Mrisho
Katika line nyingine mjomba amewaasa wasanii, kuwa makini katika
kampeni za kisiasa wanazoalikwa kuelekea uchaguzi mkuu, waungane na
viongozi wanaokubalika na wananchi
0 comments :
Post a Comment