MGOMBEA ubunge
jimbo la Segerela kupitia CUF anayeungwa mkono na vyama vyote vinavyounda UKAWA,
Julius Mtatiro, amezidi kusisitiza kuwa wananchi wanatakiwa kutatuliwa kero zao
na mbunge wao kwa kuwasikiliza, kuwafuata waliko na kuwapa majibu sahihi ya
matatizo yao na kuyatatua.
Ameeleza kuwa
njia pekee ya kufanya hivyo ni kutumia mfumo wa siku 2 + siku 1 + siku 2, yaani
katika siku tano za kazi katika wiki, yeye atazigawa kwa kutenga siku mbili
kuwa ofisini kusikiliza wananchi watakaokuwa na shida naye, siku
moja ya kutembelea wananchi jimboni kwake na siku mbili zingine ni kutumikia
wananchi kitaifa.
Ameyasema hayo
katika mkutano uliofanyika kata ya Kipawa jimbo la Segerea jijini Dar es
salaam. Pia amewataka wananchi wa jimbo la Segerea kutambua kuwa yeye ndiye
mgombea aliyeteuliwa na kupitishwa na UKAWA kugombea ubunge jimbo la Segerea, ingawa NEC imefanya
hujuma za kutomtoa mgombea wa CHADEMA katika karatasi ya kupigia kura, wakati
hagombei, ili tu kuleta mkanganyiko kwa wapiga kura na kupunguza kura kwa UKAWA.
“Kwakuwa
mnaimani na UKAWA, mimi Julius Mtatiro ndiye niliychaguliwa kupeperusha bendera
ya UKAWA kupitia CUF, na mwenzangu wa CHADEMA yeye alijitoa katika nafasi ya
kugombea ubunge kwa jimbo la Segerea na kuniunga mkono mimi. Kwahiyo mnatakiwa
kuiachana na mgombea wa CHADEMA kwani mkimchagua mtakuwa mmeharibu kura zenu,
yeye sio mgombea, mimi ndiye ninatakiwa kuungwa mkono na wanachama wote wa
CHADEMA, CUF, NCCR MAGEUZI na NLD”
Amezidi
kufafanua kuwa kwa upande wa urais ni mzee wa maamuzi magumu kupitia CHADEMA,
Edward Lowassa ndiye anapeperusha bendera ya UKAWA na ndiye anatakiwa kuungwa
mkono na vyama vyote vya CUF, CHADEMA, NCCR MAGEUZI, na NLD, ili kuleta mabadiriko
 |
Mtatiro akitoa elimu ya jinsi ya kupiga kura kwa wananchi wa jimbo la Segerea |
 |
Vijana wa bodaboda wakisikiliza sera za Mtatiro na diwani wa kata ya kipawa Kennedy, katika harakati za mtaa kwa mtaa |
 |
Mama mjasilia mali akielimishwa jinsi ya kupiga kura na kupewa sera za jinsi gani atatatuliwa kero zake kama mfanya biashara mdogo |
 |
Mama ntilie nao hajawaacha, anawafuata kila sehemu na kuwasikiliza na wao wanamsikiliza na kupata elimu ya jinsi ya kupiga kura |
 |
Vijana ndio tegemeo la UKAWA |
 |
Wajasilia mali wakionyesha kazi zao na kusikiliza nini atawafanyia yeye kama mbunge na rais wa UKAWA, Lowassa |
0 comments :
Post a Comment