TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749



Msanii Snura aiomba radhi jamii kwa kutoa wimbo na video ya “chura” iliyodaiwa na baadhi ya wadau pamoja  na serikali kuwa haina maadilli na udhalilishaji kwa jinsia ya kike. Hayo ameyasema leo, Mei 5 katika kikao na waandishi wa habari akitoa ufafanuzi baada ya hiyo jana, Mei 4 Wizara ya Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo kuifungua kutokana kudai haina maadili na zaidi, yeye kufungiwa kujihusisha na muziki mpaka pale BASATA watakapomtambua kwa kujiandikisha kwenye orodga ya wasanii wanaotambulika.
Katika kikao hicho na waandishi pia, Snura alijitokeza na meneja wa maarufu kama HK na kuonyesha cheti rasmi alichopewa na BASATA baada ya kujisajili na kuahidi kutotoa video ya namna na maudhui kama yale tena.


Msanii Snura kulia na meneja wake (HK) kushoto leo katika kikao na waandishi wa habari.





0 comments :

 
Top