Na GODWIN SIKAJULA (SJMC), DAR ES SALAAM
WANANCHI wa Kigamboni wameulalamikia uongozi wa mamlaka
ya vitambulisho vya Taifa Tanzania NIDA, kwa utaratibu mbovu juu ya zoezi zima
la upigaji picha za vitambulisho vya Taifa.
Malalamiko hayo yametolewa jana katika ofisi za NIDA
zilizoko Kigamboni ambako zoezi la upigaji picha lilipamgwa kufanyika kwa
wananchi waishio, Tungi, Vijibweni, Kigamboni, Mjimwema, Somanjila, Kimbiji,
Kisarawe, Pemba mnazi, na Kibada.
Wakitoa malalamiko yao wanchi hao walieleza kuwa, mwanzo
kila mtu alikuwa anapiga picha katika ofisi za kata yake, lakini mnamo tarehe
22 Julai mwaka huu zoezi hilo lilisitishwa na kuwataka Wananchi kwenda moja kwa
moja katika ofisi za NIDA Kigamboni na ndiko watakako piga picha hizo.
“Tulipo kuja hapa NIDA wakatuambia tuje tarehe 29 Julai
ambayo ndiyo leo, lakini chakushangaza tumefika hapa tangu asubuhi hakuna zoezi lolote linalo endelea wakati sisi
tumefunga shughuli zetu na kuna wengine ni Wanafunzi wamesafiri kutoka mikoani,
na majibu yao
wao wanasema tuondoke hadi tutakapo pigiwa simu”, alisema Pascal Faustine.
Akizidi kueleza juu ya mfumo mzima wa pale, mmoja wa
wananchi Peter Amos alisema hakuna utaratibu maalumu wa kuwaeleza Wananchi nini
cha kufanya zaidi ya kuulizana wao wenyewe.
Kwa upande mwingine viongozi waliopo katika ofisi za NIDA
walikataa kuzungumzia malalamiko hayo hadi alipo tafutwa kwa njia ya simu Afisa
habari wa NIDA William Thomas na kuzungunzua jambo hilo.
“Zoezi linaendelea na litazidi kuendelea, isipokuwa
kutokana na uwingi wa watu hatuwezi kuwahudumia watu zaidi ya 1000 na ndio
maana tukaamua kwamba, tutatoa majina ya kila mtu na tarehe ya kuja kupiga
picha hizo ili kuwa na watu wachache tunaoweza kuwahudumia”, alusema Thomas.
0 comments :
Post a Comment