TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749


Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya UYUI mkoani TABORA imethibitisha tukio la ajabu la kuinuka kwa mti aina ya MKALYA ulioanguka kwa upepo mkali zaidi ya miaka mitano iliyopita na kuwataka Wananchi wa kijiji CHESA kuulinda mti huo. 

Mti huo unakuwa ni mti wa pili kuinuka wenyewe ndani kipindi cha mwezi mmoja katika Kata ya UFULUMA wilayani UYUI, baada ya mti aina ya MSUFI uliokuwa umeanguka na kulala chini kwa zaidi ya miaka mitatu kuinuka wenyewe Oktoba Kumi na Tano mwaka huu. 

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya TABORA{UYUI} ANSELIN TENDWA na Afisa Utamaduni wa wilaya hiyo DAUD DANGUCHE wamesema watawasiliana na Watafiti ili waende kuutafiti mti huo. 

Wananchi wa kijiji hicho wamesema mti huo unatumika kwa tiba ya asili na wameiomba Serikali iwajengee uzio kuzunguka eneo hilo kwa ajili ya maonyesho

0 comments :

 
Top