TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749



Na Mayunga Jackson           
Nikiwa wiki zima toka nifike shinyanga Mjini na kutembea wilaya za karibu kama vile Kishapu mkoani Shinyanga mengi nimejionea, kikubwa ni kiu ya watanzania wa mkoa wa shinyanga kuchoshwa na CCM.
Nikianza na Shinyanga mjini nimeshuhudia mgombea wa CHADEMA Ndg Katambi, anaungwa mkono na wananchi wa tabaka lote na rika lote hapa shinyanga mjini nikiwa maeneo ya Ngokoro na Bugweto, nilishuhudia watu wakisema mgombea wa CCM  Ndg Masele, watu wanadai hata uchaguzi uliopita mwaka 2010 zengwe lilitawala katika ushindi wake, hivyo mwaka huu kweupee, wana wa Shinyanga watatumia vichinjio vyao watamkata.
Pengine CHADEMA ina cha kujivunia kutokana na mchango mkubwa wa marehemu Bob Nyanga Makani, kwa kukifanya chama hiki kupendwa na maelfu ya watu hapa shinyanga mjini. Hivyo ninakila sababu ya kuamini mwenyekiti wa BAVICHA Ndg Katambi, ataibuka kidedea kwa Masele                   
Kwa upande wa Kishapu wilaya anayotokea mbunge anayemaliza mda wake wa CCM Ndg Sueleman Nchambi, hali ya maisha bado inatisha sana nimetembelea kata nne kati ya ishirini, tatizo kubwa ni maji, wananchi hawana hata visima vya kata. Maji ni shida, wanachimba maeneo na wanatumia maji na mifugo, huduma ya afya ni mbaya kupindukia nimetembelea kata ya Itilima, Talaga, Bunambiyu na Ukenyenge, kiukweli, Suleman Nchambi, hajawatendea haki wana kishapu. Pengine nikipata bahati ya kuonana nae ntapaza sauti kwa niaba ya wana Kishapu nimuulize fedha za mfuko wa maendeleo ya jimbo amezitumia kwa mradi gani?? na kipi akiwa kama mbunge anayemaliza mda wake angejivunia kwa kata tajwa hapo juu.                    
Kwa upande wa mabadiliko wanakishapu wanahitaji mabadiliko na wameshachoshwa na CCM, kwa vijiji kadhaa nilovyotembelea nimeona na nikapata hamasa kufuatia matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa Chadema wamefanya vizuri katika vijiji vingi Kishapu.                       
Nnachokiona kwa sasa nguvu kidogo tu inahitajika kumwongezea nguvu Mgombea ubunge Chasema, Ndg Mpendazoe, awafikie wananchi wengi wa kishapu huku akiahidi kutatua kero za maji basi Sueleman Nchambi kweupee.       
Lowasa ameamsha hisia za watanzania waliochoshwa na utawala wa chama cha mapinduzi hivyo kila sehemu wapo tayari. 
Wito wangu kwa vijana wezangu wenye nia ya dhati na maendeleo ya taifa letu, tutembee tuende vijijini tutazame matatizo ya watanzania ndo tuje tujikaze na aibu yetu huku tukisema CCM oyeeee. Vinginevyo huu usaliti tunaoufanya ni dhambi kubwa mbele ya mungu.
CCM Ilipotufikisha bhaasi jamani tutoeni fursa kwa UKAWA. Viva Mabadilikoooooooooooo Lowassaaaaaaaaaa.

0 comments :

 
Top