TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749

Zimetokelezea
Nilikuwa napita barabara ya Kilwa, nikaktana na kundi kubwa la watoto wakiingia Chuo cha Polisi Kurasini,nilipoulza kulikoni nikaambiwa, ni halaiki ya watoto wazalendo wakijiandaa na sherehe za Muungano. 

Kuwaangalia wote ni watoto wa maskini. Swali la kujiulza, mkuu wa kaya na Serikali yake, wanajimwambafy kila siku kuwa ni viongozi wazalendo, tena wengine hadi wanalala na maskafu shingoni yenye rangi za bendera ya taifa, watoto wao mbona hawashiriki katika hizi halaiki kama kweli wana uzalendo? 

Kwa mtizamo wangu litakuwa jambo la maana sana kama tutamuona binti wa Kikwete, watoto wa Pinda, Nchemba, Makinda, Komba, na wengineo wote wanaojiita wazalendo ili watoto wao waige uzalendo huu, vinginevyo huo ni unafiki tu. Karibuni wadau kwa mawazo, nikosoeni kama siko sahihi

Chanzo jamii forum

0 comments :

 
Top