TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749

Mzazi mwenzie na Aunty Ezekiel huyu hapa.
Hatimae star wa filamu Bongo Aunty Ezekiel amevunja ukimya wa kwamba ni nani baba wa mtoto wake (Cookie).
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Aunty alionesha mchoro mpya “tattoo” aliyochora mgongoni ikisomeka jina la mwanae Cookie na mzazi mwenzie “Dancer” wa Diamond Mose Iyobo.
Mara kadhaa kumekuwa na taarifa na madai mbalimbali, yakikanganya ni nani hasa baba wa mtoto wa “mbongo muvi” huyo kati ya mumewe Sunday Demonte na kichuna wake mpya Mose Iyobo.
Kwa mujibu wa tattoo hiyo, imethibitishwa wazi kwamba Iyobo ndiye hasa mlengwa na mmiliki halali wa familia hiyo.

0 comments :

 
Top