Chama cha wananchi (CUF), kimesema hakikushiriki kikao cha jana cha
UKAWA kutokana na sababu za kikatiba za ndani za chama hicho kwa sababu
wao kama chama bado wanajadiliana ili kuafikiana kwa maslahi mapana ya
taifa.
Akizungumza leo Jijini Dar es Salaam Naibu Katibu Mkuu wa
chama hicho Bara Mhe. Magdalena Sakaya amesema kwa sasa wamekuwa na
vikao vinavyojadili kwa upana juu ya namna watakavyogawana madaraka
endapo wakishinda uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba.
Sakaya amesema wanachikifanya ni sawa na vyama vingine vinavyofanya na
kukanusha kuwa sio kweli kwamba CUF wamejitoa katika umoja huo.
0 comments :
Post a Comment