Dodoma/Z’bar. Wakati vikao vya juu vya CCM vya kuchuja wagombea urais vikianza leo, hofu na wasiwasi umezidi kutanda miongoni mwa wagombea, viongozi na wanachama wa chama hicho kuhusu namna ya kuikabili minyukano baina ya wagombea hao na kibarua cha Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa miongoni
mwa mambo yanayoleta hofu na kusababisha presha kuongezeka kila kukicha
ni woga wa kufanya makosa katika uteuzi wa ndani, hali inayoweza
kukigharimu chama hapo baadaye hasa kutokana na kuongezeka nguvu ya
upinzani.
Kutokana na hali hiyo kumekuwa na shinikizo kutoka
katika makundi mbalimbali chama hicho kuwa makini kumteua mgombea
anayekubalika, msafi na mwenye kuchagulika ambaye atatoa ushindani kwa
wagombea wa upinzani, hasa Ukawa.
Vilevile, kumekuwapo na wasiwasi wa baadhi ya
wagombea kutishia kukihama chama hicho endapo majina yao yatakatwa,
jambo ambalo pia linakiweka njia panda.
0 comments :
Post a Comment