Chalinze. Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Damian Lubuva amesema hadi sasa wameshaandikisha wapigakura zaidi ya milioni kumi na moja kati ya milioni 24 wanaotarajiwa kuandikishwa nchini kote.
Kutokana na idadi hiyo, Jaji Lubuva amesema NEC ina uhakika wa kukamilisha kazi hiyo ya uandikishaji mapema Agosti mwaka huu.
Alisema hayo jana alipokuwa Msoga, Chalinze
wilayani Bagamoyo wakati akitoa taarifa kwa Rais Jakaya Kikwete ambaye
alikuwa mmoja wa wananchi wa eneo hilo waliojitokeza kujiandikisha
kwenye Daftari la Wapigakura, ikiwa ni siku ya kwanza ya kuanza kazi
hiyo mkoani Pwani.
Alimueleza Rais Kikwete kuwa licha ya changamoto
kadhaa zilizojitokeza katika mchakato huo, hali ya uandikishaji
ilipofikia nchini hadi juzi ni nzuri na matumaini ya NEC ni kukamilika
mapema Agosti kwa kuwafikia walengwa wote waliokusudiwa.
Awali, Jaji Lubuva alikuwa akisema kuwa kazi hiyo
ingekamilika Julai na hata uandikishaji uliposogezwa mbele kwa jiji la
Dar es Salaam na Pwani, NEC ilisisitiza kuwa utakamilika kabla ya mwisho
wa Julai.
“Mheshimiwa Rais, pamoja na changamoto nyingi na
kelele nyingi zilizokuwa zikisikika huku na kule, tayari tumeandikisha
watu 11,248,198 mpaka jana (juzi) kati ya lengo tulilojiwekea la
kuwafikia watu kati ya milioni 21 mpaka 23 na mikoa iliyokuwa tayari
imekamilisha zoezi hili ni 13, bado kumi na moja ambayo nayo
nakuhakikishia itakamilisha na mapema mwezi Agosti kazi hii
itakamilika,” alisema Jaji Lubuva.
Chanzo Mwananchi
Chanzo Mwananchi
0 comments :
Post a Comment