TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749

Umoja wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya wananchi UKAWA leo umetangaza rasmi kususia vikao vya bunge vilivyobaki kwa madai ya kukiukwa kwa kanuni za bunge.
Akitangaza msimamo huo mjini Dodoma katika mkutano na waandishi wa habari, kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni Mh. Freeman Mbowe amesema wabunge wote kutoka katika vyama vinavyounda umoja huo hawataingia tena bungeni licha ya baadhi yao kuwa hawajaadhibiwa.
Wakati huo huo Bunge mchana huu limepitisha miswada miwili iliyokuwa imebaki baada ya mmoja kupitishwa jana.
miswada iliyopitishwa leo ni wa sheria ya usimamizi wa mapato yatokanayo na gesi na mafuta pamoja na muswada wa sheria ya uwazi na uwajibikaji katika uchimbaji bila ushiriki wa wabunge wa upinzani.

0 comments :

 
Top