TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749

Bingwa wa dunia wa mbio za  kufukuza upepo za mita 100 kwa upande wa wanaume,Usain Bolt wa Jamaica, ameibuka na kuwapiku wapinzani wake wakuu alipohifadhi taji lake la dunia mbele ya umati mkubwa uliojitokeza kushuhudia fainali hiyo katika uwanja wa kimataifa Birds Nest jijini  Beijing  huko China.
Bolt alitoka nyuma na kuukata utepe katika fainali iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu  na watu wengi zaidi katika mashindano ya riadha duniani yanayoendelea nchini China.
Licha ya kupigiwa upatu kuwa mashindano magumu kwa kujumuisha majina yote tajika yakiwemo wanaridha wakuu wa mbio hizo, Asafa Powell, Mmarekani Tyson Gay na Justin Gatlin,ambaye amepigwa marufuku mara mbili kwa kupatikana na hatia ya matumizi ya dawa za kuongeza nguvu,Bolt alikata utepe na kuibuka kidedea.
Gatlin alimaliza chini ya nukta moja nyuma ya Bolt alimaliza muda wa sekunde 9.79.
Raia wa Canada, Andre de Grasse na Mmarekani Trayvon Bromell walitia nanga muda wa sekunde 9.92 na kutunzwa medali ya shaba.

Gatlin alikuwa na rekodi ya kushiriki mbio 28 bila ya kushindwa msimu huu na japo alikuwa amepigiwa upatu kuibuka mshindi huko Beijing,Kulikuwa na hofu kubwa yakuwa endapo angeibuka mshindi basi ushindi wake ungelitia doa jina la mchez o wa riadha ambao umekumbwa na madai hivi majuzi ya matumizi makubwa ya madawa za kuongeza nguvu yaliyopigwa marufuku.

Bolt atakumbukwa kwa kuibuka kidedea kati8ka mbio za matimko alipozoa medali za dhahabu katika mbio za mita 100 na mita 200 katika mashindano ya olimpiki mwaka wa 2008 huko huko Beijing.
Bingwa wa dunia wa mbio za kufukuza upepo za  mita 100 kwa upande wa wanaume,Usain Bolt wa Jamaika, ameibuka na kuwazidi wapinzani wake wakuu alipoibuka na taji lake la dunia mbele ya umati mkubwa uliojitokeza kushuhudia fainali hiyo katika uwanja wa kimataifa Birds Nest jijini Beijing huko  China.
Bolt alitoka nyuma na kuukata utepe katika fainali iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu  na watu wengi zaidi katika mashindano ya riadha duniani yanayoendelea nchini China.
Licha ya kupigiwa upatu kuwa mashindano magumu kwa kujumuisha majina makubwa  yakiwemo ya  wanaridha wakuu wa mbio hizo, Asafa Powell, Mmarekani Tyson Gay na Justin Gatlin, ambaye amepigwa marufuku mara mbili kwa kupatikana na hatia ya matumizi ya dawa za kuongeza nguvu, Bolt alikata utepe na kuibuka kidedea.
Kwa Gatlin ambaye  alimaliza chini ya nukta moja nyuma ya Bolt alitimiza muda wa sekunde 9.79.
Raia wa Canada, Andre de Grasse na Mmarekani Trayvon Bromell walitia nanga kwa muda wa sekunde 9.92 na kutuzwa medali ya shaba, Gatlin alikuwa na rekodi ya kushiriki mbio 28 bila ya kushindwa msimu huu na japo alikuwa amepigiwa upatu kuibuka mshindi huko Beijing, ambapo kulikuwa na hofu kubwa yakuwa endapo angeibuka mshindi basi ushindi wake ungetia doa mchezo wa riadha ambao umekumbwa na madai hivi majuzi ya matumizi makubwa ya madawa za kuongeza nguvu yaliyopigwa marufuku.
Bolt atakumbukwa kwa kuibuka kidedea katika mbio za kukimbiza upepo alipoibuka na medali za dhahabu katika mbio za mita 100 na mita 200 katika mashindano ya Olimpiki mwaka wa 2008 huko huko jijini Beijing.

0 comments :

 
Top