TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749


Mbunge aliyemaliza muda wake, Makongoro Mahanga amewataka wananchi kuachana na CCM kwani viongozi wa CCM wanamapembe hawataki kufanya kazi kwa kushirikiana, hii yote ni kwasababu ya wizi hasa madiwani, wakuu wa wilaya na mikoa.

Ameyasema hayo leo kwenye mkutano wa UKAWA, wa kumnadi mgombea ubunge wa jimbo la Segerea, Julius Mtatiro. Amesema kuwa yeye anauzoefu  kwa viongozi hao kuwa na viburi hasa katika kushughulikia matatizo ambayo yanatakiwa kushughulikiwa kwa pamoja hivyo wananchi wasifanye makosa ya kuichagua CCM.

Mtatiro akiwa na Makongoro pamoja na mgombea udiwani

“Viongozi wengi wa CCM wanamapembe na nimabubu, hawataki kushirikiana na wabunge kutatua matatizo ya wananchi. Madiwani hawataki kumshirikisha mbunge kwenye vikao vyao, wakuu wa wilaya na mikoa hawataki kutekeleza maombi ya mbunge na hata mameya ndio wanashirikiana na madiwani kuiba mali za uma. Yote haya nikwasababu ya wizi uliokithiri. Mnataka kumchgua mgembea ubunge wa CCM kata ya Segerea, wakati alikuwa diwani na hajawahi hata kutoa hoja kule almashauri, Je, bungeni ataweza ? yeye alikuwa anasusa susa tu na hii ndio sifa ya viongozi wa CCM kutokuwa na hoja” alisema Makongoro.

Alisema yeye amehama na mipango yote ambayo alianza na Mh Edward Lowassa, ambayo ilikuwa inawahusu madereva bodaboda kukopeshwa pikipiki kwa riba ndogo na wakina mama kwenye vikoba pia kupewa mikopo yenye masharti sawa na bure. Alisisitiza kuwa mpango huo ni endelevu na amemkabidhi Julius Mtatiro na punde tu atakapochaguliwa atawakabidhi wananchi.

Kwa upande wake Mtatiro alisema kuwa matatizo makubwa anayoenda kuyatatua endapo atapigiwa kura ya kuwa mbunge wa Segerea, ni migogoro ya aridhi, ukosefu wa soko, miundombinu mibovu pamoja na kuhakikisha mikopo inayotengwa kwaajili ya vijana na wakina mama inawafikia na bila kuwasahau vijana.

“Najua serikali ya CCM imewasababishia kukosa fedha nyingi sana kutokana na fedha hizo kuliwa na wachache. Mlitakiwa kupata kila kata zaidi ya miloni 400hadi 500 kwaajili ya maendeleo, na mlitakiwa kupata milioni 220 kwaajili ya mikopo kwa vijana na wakina mama. Zote hizo hazijawafikia kwakuwa viongozi wa CCM wamekuwa wakila fedha hizo. Je! milioni 500 haitoshi kujengea masoko na miundombinu ya shule na vituo vya afya na vifaa vyake? hizi zinatosha kabisa” alisema Mtatiro.
Mtatiro akiwa na mgombea udiwani kata ya Tabata, Assenga

Mtatiro amewahutubia pia wananchi wa kata ya Tabata, ambako aliwaambia wananchi kuwa anajua matatizo ya bodaboda kuzuiliwa kuingia mjini, tatizo la mitaro na ukosefu wa maji wakati maji yanapitishwa na mabomba kwenda Masaki wakati ni kazi ndogo tu, ya kuchimba visima vitakavyo sambaza maji kwa wannchi.

Pia aliwahakikishia wananchi ahadi ya elimu bure inatekelezeka na wananchi wanatakiwa kuichagua UKAWA ili kufaidi kuwasomesha watoto wao bure kuanzia chekechea hadi vyuo vikuu, na wazazi wausubiri kuhangaikia sare za shule tu.

Mtatiro akiwa na mgombea udiwani kataya Kinyerezi (Greyson Celestine) pamoja na Makongoro wakitoa elimu jinsi ya kupiga kura

Kama kawida yake kila kona ya mtaa, kuwe na sherehe anawafikia na kuwapa elimu juu ya kupiga kura na kumwaga sera

Haachi kula nao

Wananchi wa Tabata wakionyesha style ya Magufuli ndio nani...?

0 comments :

 
Top