TUMA HABARI YOYOTE ULIYONAYO KWENDA zimetokelezea@gmail.com AU Whatsapp No 0716790749

Dr S Kiria aliyekuwa mkuu katika kitengo cha IT Tehama kabadilishwa zikiwa zimebaki siku chache za upigaji kura. Tunajiuliza inakuwaje abadilishwe leo.
Mtamkumbuka mara nyingi ndie alikuwa akihojiwa na vituo mbali mbali za TV na wanahabari kuhusu maswala ya BVR na aliweza kujieleza vizuri na kukithi matakwa ya wanahabari na wananchi kwa ujumla.
Habari kutoka ndani zinasema Dr Kiria amepozwa na kabila lake kwani yeye ni wa kaskazini. Ivi sasa katika tume ukionekana ni wa kaskazini unapigwa chini, huo ndio mkakati kutoka Magogoni.
Wanyetishaji wanazidi kusema hata Jaji Lubuva alikuwa aondolewe kwenye nafasi yake. Jaji aligoma kuachia ngazi akisema kwanini aondolewe leo wakati siku za uchaguzi zimebaki chache???. Akawauliza kwanini hawakumwondoa mwaka jana???
Hayo yote yanatokana na tume ya mwaka huu kutokubali baadhi ya matakwa ya CCM.
Matokeo aliyatoa Makamba na ya jana Twaweza na leo mkurugenzi wa IT kuondolewa ni jitahada za kuandaa namna ya kuchakachua kura.
Wafanyakazi wengi wa tume wamechanganyikiwa na hawaelewi haya yanayotokea sasa. Kwani wanasema Kiria alikuwa anaimudu idara yake na alikuwa mtetezi wa wanyonge.
Chanzo. Julius Mtatiro

0 comments :

 
Top