Rapa mwenye heshima kubwa na mwenye kujiamini siku zote Marshall Bruce Mather a/k/a Eminem amemuandikia baraua ya heshima Mama mzazi wa marehemu rapa Tupac Amaru Shakur a/k/a 2Pac.
Barua hiyo aliiandika kwa mkono wake alimtumia Afeni Shakur ambaye ni Mama wa 2 Pac na kuweka wazi ni jinsi gani Eminem anavyomkubali na kumuheshimu marehemu mwanaye.
Katika barua hiyo Eminem aliandiaka maneno yenye maana ifuatayo “ Tangu nilipokuwa na umri wa miaka kumi, hata kabla sijakutana na Dr. Dre nilianza kujifunza kuandika, mpaka leo nipo vizuri na najiamini na kuweza kusema lolote mbele ya dunia hii. Yote haya na ujasiri huu nimejifunza kutoka kwa 2Pac ambaye mpaka sasa hakuna aliyeweza kuifikia historia na heshima yake ”.
0 comments :
Post a Comment